Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 53 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 461 2019-06-26

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:-

Mji wa Kibaha unakua kwa kasi hivyo mahitaji ya Watumishi yameongezeka ikiwemo Watendaji wa Mitaa, Maofisa Mifugo, Walimu pamoja na Watumishi:-

Je, ni lini Serikali itatoa kibali cha ajira na kuajiri Watumishi pungufu ili kuleta ufanisi zaidi katika Halmashauri ya Mji wa Kibaha?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Silvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa ikama ya mwaka wa fedha wa 2018/2019 Halmashauri ya Mji wa Kibaha ilikuwa na uhitaji wa Watumishi 1,854 ambapo waliopo ni 1,713 na upungufu ni watumishi 140 sawa na asilimia 7.7. Hivyo, Halmashauri ya Mji wa Kibaha ni miongoni mwa Halmashauri zenye tatizo dogo la upungufu wa watumishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuajiri Watumishi wa Kada mbalimbali na kuwapanga kwenye halmashauri kwa kuzingatia mahitaji ya halmashauri kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha. Ahsante.