Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 53 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 460 2019-06-26

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA (K.n.y. MHE. SEIF K. GULAMALI) aliuliza:-

Wilaya ya Igunga ilipata ufadhili wa Benki ya Dunia wa ujenzi wa Vituo vya Afya vya Simbo, Ziba, Chomachankola na Igurubi ambapo Vituo vya Afya vya Ziba, Chomachankola na Igurubi vimekamilika na vifaa tayari vipo japo majengo na vifaa katika Kituo cha Afya cha Chomachankola na Igurubi bado havijaanza kufanya kazi; Kituo cha Afya cha Simbo bado hakijakamilika na vifaa havipo na Wafadhii walishakabidhi Halmashauri bila kukamilisha ujenzi huo:-

Je, Serikali inachukua hatua gani kujua nini kilichojificha juu ya Mradi huo kukabidhiwa bila kukamilika?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Seif Khamis Gulamali, Mbunge wa Manonga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa Wilaya ya Igunga ilipata ufadhili wa Benki ya Dunia kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya Simbo, Ziba, Chomachankola na Igurubi. Sababu kuu ya kushindwa kukamilika kwa miradi hiyo kwa wakati ilitokana na makadirio ya chini ikilinganishwa na gharama halisi za kukamilisha ujenzi. Ili kukamilisha ujenzi wa Vituo hivyo kwa kuzingatia ramani mpya, Serikali ilitoa jumla ya shilingi milioni 800 kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya Simbo na Igurubi ambapo kila kituo kilipatiwa shilingi milioni 400.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya cha Simbo kimekamilisha ujenzi wa majengo ya upasuaji na nyumba ya mtumishi na sasa vifaa tiba vinaendelea kuletwa. Aidha, Kituo cha Afya Igurubi kinaendelea na ujenzi wa majengo manne ambayo ni Maabara, Jengo la Wazazi, Jengo la Kufulia na Jengo la Kuhifadhia maiti. Majengo yote haya yapo katika hatua za ukamilishaji.