Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 52 Water and Irrigation Wizara ya Maji 456 2019-06-25

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA (K.n.y MHE. DAVID E. SILINDE) aliuliza:-

Je, ni upi mpango wa sasa wa kutatua kero ya maji katika Jimbo la Momba?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Kwa niaba ya Mheshimwa Maziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa David Ernest Silinde, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mpango wa sasa wa Serikali wa kutatua kero ya maji katika Jimbo la Momba ni kupitia utekelezaji wa Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDP) ambayo inatekelezwa pia katika Halmashauri zote nchini. Programu hiyo imelenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na endelevu ya majisafi na salama.

Mheshimiwa Spika, kupitia pragramu hiyo, tayari katika Wilaya ya Momba Serikali imekamilsha miradi ya maji mitano katika vijiji vya Namtambala, Itumbula, Iyendwe, Mnyuzi na Chilulumo ambapo jumla ya wananchi 20,271 wanapata huduma ya maji.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2018/ 2019, Halmashauri ya Wilaya ya Momba imetengewa kiasi cha Sh.1,744,000,000 kwa ajili ya uchimbaji wa visima, usanifu na ujenzi wa miundombinu ya maji. Utekelezaji wa miradi hiyo uko katika hatua mbalimbali ambapo mradi wa maji katika Kijiji cha Tindingoma, mkandarasi amesaini mkataba kwa ajili ya ujenzi; Mradi wa maji katika Kijiji cha Kitete upo kwenye hatua za manunuzi; na kwa ajili ya kumpata mkandarasi wa ujenzi wa mradi katika Kijiji cha Ikana upo kwenye hatua ya usanifu.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hatua hizo zilizochukuliwa, Serikali pia ipo katika hatua ya manunuzi ya kumpata makandarasi wa kupima na kuchimba visima katika vijiji saba (7) vya Mpapa, Samang’ombe, Kasinde, Namsinde, Chole, Nkangamo na Itelefya. Vilevile, mkandarasi huyo atafanya usanifu wa mradi wa maji utakaotumia chanzo cha Mto Momba kwa kuhudumia vijiji 21 vya Ivuna, Lwate, Mkomba, Ntungwa, Kalungu, Sante, Tontela, Kaonga, Nsanzya, Chuo, Namsinde I, Kasanu, Masanyinta, Senga, Mweneemba, Makamba, Naming’ongo, Yala, Muuyu, Usoche na Makao Makuu ya Wilaya ya Momba.