Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 52 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 448 2019-06-25

Name

Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuitengeneza kwa kiwango cha kupitika muda wote wa mwaka barabara inayounganisha Kijiji cha Mbelezungu na Kijiji cha Majeleko vyote vikiwa ndani ya Kata ya Majeleko?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joel Mwaka Makanyaga, Mbunge wa Chilonwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mbelezungu – Majeleko yenye urefu wa kilometa 10 imeingizwa kwenye mtandao wa barabara zinazohudumiwa na Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) na hivyo kukidhi vigezo vya kufanyiwa matengenezo kupitia fedha za Mfuko wa Barabara. Aidha, tathmini ya barabara hiyo imefanyika na kubaini zinahitajika shilingi milioni 288.9.

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuifanyia matengenezo barabara hiyo kulingana na upatikanaji wa rasilimali fedha.