Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 51 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 442 2019-06-24

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:-

Kituo cha Polisi Nkome kina Askari wa kiume pekee hivyo hata huduma kwa akina Mama ikiwemo upekuzi hufanywa na Askari wa kiume:-

Je, ni lini sasa Serikali itapeleka askari wa kike katika kituo hicho?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma, Mbunge wa Geita Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, vituo vidogo vya Polisi Nkome, Nyamboge, Kakubilo na Nzela ni vituo vilivyo katika maeneo ambayo yanakaribiana na kutokana na changamoto za mazingira magumu na ukosefu wa mazingira rafiki, vituo hivi kwa sasa havina Askari wa Kike ambao wanaishi na kufanya kazi. Hata hivyo, vituo hivi kupata doria maalum kila mara kutoka Kituo Kikuu cha Polisi Wilaya ya Geita ambapo Askari wa Kike na Kiume hufika na kutoa huduma za kiusalama.

Mheshimiwa Naibu Spika, endapo kuna mtuhumiwa wa kike amekamatwa katika vituo hivi vidogo hufanyika utaratibu wa kumpata mgambo wa kike wa eneo hilo au mwanamke yeyote mtu mzima mwenye busara anayepatikana kwa urahisi katika maeneo hayo kama ambavyo PGO 288 (8), (a) inavyoelekeza, ambapo hufanya upekuzi kwa mtuhumiwa huyo mwanamke.

Mheshimiwa Naibu Spika, siyo kweli kuwa watuhumiwa wa kike hupekuliwa na Askari wa Kiume, Serikali itapeleka Askari wa Kike pindi mazingira ya utendeji kazi hususan makazi yatakapokuwa yameboreshwa.