Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 51 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 434 2019-06-24

Name

Sabreena Hamza Sungura

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. SABREENA H. SUNGURA) aliuliza:-

Kituo cha Afya kilichopo Kigoma Ujiji Manispaa kinahudumia wakazi zaidi ya elfu arobaini katika Kata kumi na moja za Manispaa lakini kina kinakabiliwa na ukosefu wa Chumba cha theatre, X-ray pamoja na Ultra Sound:-

Je, ni lini Serikali itakipatia Kituo hiki vifaa hivyo ili kusaidia wananchi hao wanaohudumiwa na Kituo hicho?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sabreena Hamza Sungura Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji ina jumla ya vituo vya kutolea huduma za afya 24, hospitali mbili, vituo vya afya vinne, Zahanati 17 na Kliniki moja. Katika mwaka wa fedha 2018/2019 Halmashauri imepanga kutumia shilingi milioni 45 za bakaa iliyopo MSD kununua mashine 1 ya Ultra sound.

Mheshimiwa Naibu Spika, Vilevile katika mwaka wa fedha 2019/2020 Kituo kimetenga kiasi cha shilingi milioni 15.4 kupitia fedha za mradi wa malipo kwa ufanisi (RBF) kwa ajili ya ukarabati wa chumba kinachotumika kwa huduma za mionzi.