Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 50 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 427 2019-06-21

Name

Rashid Mohamed Chuachua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Primary Question

MHE. DKT. RASHID M. CHUACHUA aliuliza:-

Mwaka 2017/2018 kulitokea mauaji ya vijana wa bodaboda katika Wilaya ya Masasi ambapo vijana wanaokaribia kuwa zaidi ya kumi wameuwawa kikatili na kunyang’anywa pikipiki:-

Je, nini kauli ya Serikali kuhusu matukio haya katika Wilaya ya Masasi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Rashid Mohamed Chuachua, Mbunge wa Masasi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, siyo kweli kuwa kulikuwa na mauaji ya vijana zaidi ya 10 katika Wilaya Masasi. Kwa mwaka 2017/2018 kulikuwa na matukio manne ya mauaji yaliyotokea na kuripotiwa katika vituo vya Polisi Wilaya ya Masasi. Hata hivyo, Serikali kupitia Jeshi la Polisi imeendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kutokomeza uhalifu huo kwa kuwakamata watuhumiwa wote ambao wamekuwa wakijihusisha na uhalifu wa aina mbalimbali ikiwemo mauaji. Hatua hizi ni pamoja na kufanya doria na misako ya mara kwa mara katika maeneo tofauti katika Wilaya ya Masasi kutoa elimu kwa waendesha bodaboda juu ya tahadhari ya kuwabeba abiria usiku na kushirikisha jamii yote katika kuwafichua wahalifu walio kati yao ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.