Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 50 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 425 2019-06-21

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI (K.n.y MHE. STANSLAUS S. MABULA) aliuliza:-

Magari mengi ya Serikali yanafanyiwa service kwenye gereji kubwa hapa nchini hii imekuwa tofauti kwa magari yanayomilikiwa na Jeshi la Polisi:-

Je, Serikali haioni kuwa upo umuhimu wa kuwa na maeneo ya kutengeneza na kurekebisha magari ya Polisi ili kuliimarishia vitendea kazi.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula, Mbunge wa Nyamagana kama ifutavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi linayo karakana kuu ya kutengeneza na kurekebisha magari yake iliyopo barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam. Karakana hii ina matawi katika kila Mkoa nchini nzima, matawi hayo kufanya kazi kwa utaratibu wa Jeshi la Polisi chini ya Komandi ya karakana kuu iliyopo Dar es Salaam ambako kuna mafundi wenye ujuzi mkubwa. Aidha, Jeshi la Polisi kupitia makubaliano ya kimkataba kuna baadhi ya magari ya Jeshi la Polisi hutengenezwa katika karakana za wazabuni waliokubaliana baada ya kupata kibali cha TEMESA.