Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 46 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 387 2019-06-17

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. HAWA S. MWAIFUNGA) aliuliza:-

Ajali za barabarani bado zimekuwa tishio kubwa kwa maisha ya Watanzania, kutokana na ajali hizo tunapoteza nguvu kazi ya Taifa na familia nyingi zinabaki zikitaabika.

Je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na ajali hizo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Subira Mwaifunga, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na athari kubwa za ajali za barabarani kwa Taifa Serikali ina mkakati madhubuti wa kupambana na tatizo hili. Mikakati hiyo ni pamoja na kuongeza wigo wa elimu ya usalama barabarani kwa watumiaji wa vyombo hivyo kwa njia ya redio, luninga na machapisho na vipeperushi.

Aidha, mikakati mingine ni kuboresha mifumo ya utendaji kazi maeneo ya ukaguzi wa mabasi na maroli, mfumo wa ufuatiliaji wa magari barabarani na mfumo wa uwekaji nukta katika leseni za madereva utakaodhibiti tabia za madereva wazembe.

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia Baraza la Taifa la Usalama Barabarani Serikali ilibuni na kutekeleza mikakati hii ya kupunguza ajali barabarani ambao katika awamu tatu zilizotekelezwa mpaka sasa umefanikiwa kupunguza ajali kwa asilimia 43. Aidha, awamu ya nne ambayo inaendelea kutekelezwa tumejipanga kupunguza ajali kwa asilimia 35.