Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 46 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 384 2019-06-17

Name

Juma Kombo Hamad

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. JUMA KOMBO HAMAD aliuliza:-

Ni muda mrefu Serikali ilikuwepo kwenye mchakato wa kupata Vazi la Taifa.

(a) Je, Serikali imefikia hatua gani ya mchakato huo?

(b) Je, ni lini Watanzania wategemee kuwa na Vazi la Taifa?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Juma Kombo Hamad, Mbunge wa Wingwi lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mchakato wa Vazi la Taifa ulianza mwaka 2003/2004 na kufufuliwa tena mwaka 2011 baada ya kuona mitindo iliyopatikana haikukidhi haadhi ya kuwa na Vazi la Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2011 Kamati ya Kukamilisha Mchakato wa Kupata Vazi la Taifa iliteuliwa ambapo upatikanaji wa Vazi la Taifa ulipitia jatika hatua kadhaa ambazo Wizara ilishirikisha wabunifu na wanamitindo kwa lengo la kushirikisha wadau wa fani hizo ili kupata Vazi la Taifa litakalotambulisha Taifa letu.

Baada ya kamati kumalizia kazi yake ilikabidhi Wizarani taarifa na mapendekezo kuwa Vazi la Taifa litokane na aina ya kitambaa na siyo mshono.Aidha, aina ya vitambaa kwa vazi hilo ilipendekezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Baraza la Mawaziri iliagiza kwamba jamii iachiwe huru kuchagua aina ya vazi ambalo litatokana na mageuzi ndani ya jamii yenyewe na isiwe uamuzi wa Serikali. Wizara ilitoa taarifa kwa maamuzi yaliyofikiwa na Serikali kwenye vyombo vya habari na tovuti ya Wizara ili wananchi wajadili na waamue wenyewe kuhusu Vazi la Taifa ambalo litapendekezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, baadhi ya changamoto zilizojitokezakwa kipindi hicho ni uhamasishaji hafifu wa uvaaji wa Vazi la Taifa. Aidha walitarajia kupokea vazi na siyo kuoneshwa kitambaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya agizo la Waziri Mkuu la kuandaa Tamasha la kupata sura ya Vazi la Taifa ifikapo 30 Desemba, 2018, mchakato ulianza upya ambapo utaratibu wa ukusanyaji wa michoro, picha ya vazi au mavazi halisi kutoka kwa wabunifu kwa kila mkoa uliandaliwa kwa kuwaandikia Makatibu Tawala wa Mikoa yote, kuwapa taarifa kuhusu mchakato wa kupata Vazi la Taifa kwa kushirikiana na Maafisa Utamaduni kuhamasisha wabunifu ili waweze kuandaa, kuwasilisha michoro, picha au mavazi waliyobuni yanayoendana na asili ya mkoa husika. Aidha, Wizara imeweka mkakati maalumu kwa kushirikiana na Maafisa Utamaduni ili kuweza kupata Vazi la Taifa.