Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 46 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 380 2019-06-17

Name

Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA (K.n.y. MHE. OMARI A. KIGODA) aliuliza:-

Kuna mgogoro mkubwa wa ardhi unaondelea katika Wilaya ya Handeni ambao kama hatua za haraka hazikuchukuliwa unaweza kusababisha ugomvi mkubwa kati ya wananchi.

Je, nini tamko la Serikali katika kuzuia tatizo hilo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omari Abdallah Kigoda, Mbunge wa handeni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inawaagiza viongozi na watendaji wote wa Serikali katika Wilaya ya Handeni kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia uendelezaji wa ardhi ili kuzuia migogoro ya ardhi. Aidha, wananchi wanasisitizwa kuzingatia sheria za ardhi na kujiepusha kuvamia maeneo yasiyoruhusiwa ili kuepuka migogoro isiyokuwa ya lazima. Tathmini inaonesha ipo migogoro inayohusisha mipaka baina ya halmashauri moja na nyingine, migogoro baina ya wamiliki wa ardhi na wananchi na baadhi ya wananchi kuvamia maeneo ya ardhi yasiyoruhusiwa. Viongozi wa Mkoa wa Tanga na Wilaya ya Handeni wanaelekezwa kutatua migogoro hiyo kwa kushirikisha wananchi na kwa kuzingatia sheria za ardhi. Serikali haitasita kuchukua hatua kwa viongozi na watendaji watakaobainika kukiuka sheria za ardhi na kusababisha migogoro ya ardhi. Ahsante.