Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 45 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 375 2019-06-13

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-

Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji na Vitongoji wanafanya kazi kubwa na ngumu sana hasa Mtwara Mjini na maeneo mengine ya nchi yetu.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwalipa mishahara kama ilivyo kwa Watendaji wa Vijiji na Mitaa?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maftaha Abdallah Nachuma, Mbunge wa Mtwara Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kazi kubwa na nzuri inayofanywa na Wenyeviti wa Vijiji, Mitaa na Vitongoji katika shughuli za maendeleo. Hata hivyo, kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi wa Wenyeviti wa Serikali za Vijiji, Mitaa, Vitongoji na Wajumbe wa Serikali za Vijiji pamoja na Wajumbe wa Mitaa za mwaka 2014 zilizotolewa kupitia Tangazo la Serikali Na. 322 na Na. 323, sifa zinazomwezesha mkazi wa Mtaa, Kijiji na Kitongoji kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti au Mjumbe wa Serikali za Mitaa ni pamoja na kuwa na shughuli halali inayomwingizia kipato.

Mheshimiwa Spika, Wenyeviti wa Vijiji, Mitaa na Vitongoji siyo watumishi wa umma na hivyo hawaajiriwi na kulipwa mishahara kama ilivyo kwa Watendaji Vijiji na Mitaa. Hata hivyo, kwa kuzingatia kazi kubwa inayotekelezwa na viongozi hawa katika kusimamia shughuli za maendeleo katika maeneo yao, Serikali inawalipa posho kutokana na asilimia 20 ya mapato ya ndani ya Halmashari kwa mujibu wa Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura 290. Ulipaji wa posho ya viongozi hao unategemea hali ya makusanyo ya kila Halmashauri. Serikali inatoa wito kwa Halmashauri zote ikiwemo Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani kuthamini mchango mkubwa wa viognozi hao na kuwalipa posho kutokana na mapato ya ndani. Ahsante.