Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 44 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 374 2019-06-12

Name

Christopher Kajoro Chizza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ENG. CHRISTOPHER K. CHIZA aliuliza:-

Wafanyabiashara wa Wilaya ya Kakonko wanapenda kujisajili BRELA ili kurahisisha biashara zao na kulipa kodi stahiki lakini wengi wanashindwa kufanya hivyo kwa kukosa Vitambulisho vya Taifa

(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuharakisha zoezi la kutoa Vitambulisho vya Taifa ili wananchi waweze kuvitumia katika shughuli za maendeleo?

(b) Kuna wananchi wanaokaa katika mipaka kati ya Tanzania na nchi nyingine; je, Serikali imewawekea utaratibu gani wa kuwapa vitambulisho wananchi hao kwa haraka bila kuathiri malengo ya zoezi la utoaji wa Vitambulisho vya Taifa?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Christopher Kajoro Chiza, Mbunge wa Buyungu, lenye vipengele (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) inaendelea kukamilisha usajili wa watu wote wenye sifa kwa matarajio ya kukamilisha zoezi la uchukuaji wa alama za vidole, picha na saini za kielektroniki ifikapo tarehe 31 Desemba, 2019. Lengo la Serikali ni kununua mashine mpya za uzalishaji wa vitambulisho zenye uwezo mkubwa zaidi ili kuharakisha upatikanaji wa Vitambulisho vya Taifa. Aidha, Mamlaka imefungua dawati Maalum la usajili katika ofisi ya BRELA, usajili huu unafanyika kwa kuzingatia sifa bila kuathiri masharti ya kisheria na kikanuni yaliyowekwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kuwapa vitambulisho vya taifa kwa haraka wananchi wanaokaa mikoa ya mipakani, utaratibu wake hautofautiani na utaratibu wa kawaida wa usajili ambapo mamlaka kuhakikisha kuwa taratibu zote za usajili zimezingatiwa na hatua zote za uhakiki na ufuatiliaji wa mapingamizi zimefuatwa kikamilifu. Natoa rai kwa wananchi wote nchini kuanza taratibu za usajili mapema ili kuepusha usumbufu.