Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 44 Energy and Minerals Wizara ya Madini 372 2019-06-12

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:-

Kampuni ya Mabangu ina leseni ya utafiti wa madini katika maeneo ya Nyakafuru, Bukandwe na Kanegere Wilayani Mbogwe; kampuni hiyo inafanya utafiti kwa kushirikiana na kampuni nyingine ya Resolute lakini utafiti huo umechukua muda mrefu.

(a) Je, ni lini kampuni hizo zitafungua mgodi katika eneo lao la utafiti?

(b) Kama kampuni hizo zimeshindwa kuanzisha mgodi; je, Serikali iko tayari kuona uwezekano wa kuligawa eneo hilo kwa wachimbaji wadogo wa Wilaya ya Mbogwe?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele, Mbunge wa Mbogwe lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo ya Nyakafuru, Bukandwe na Kanegere katika Wilaya ya Mbogwe yana leseni ya utafiti mkubwa yenye ukubwa wa kilometa za mraba 17.53 inayomilikiwa na Kampuni ya Mabangu Mining Limited ambayo ni kampuni tanzu ya Resolute Tanzania Limited kupitia leseni ya utafutaji wa madini namba PL 5374/2008. Leseni hiyo ilitolewa kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya mwaka 1998 tarehe 24/10/2008 kwa kipindi cha miaka tatu ya awali.

Aidha, kulingana na Sheria ya Madini ya mwaka 2010, leseni hiyo ilihuishwa kwa mara ya kwanza kwa kipindi cha miaka mitatu na mara ya pili kwa miaka miwili.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile mwaka 2016 kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya Mwaka 2010, leseni hiyo iliongezewa muda (extension) kwa kipindi cha miaka miwili ili kukamilisha kazi ya upembuzi yakinifu kabla ya kuwasilisha maombi ya leseni ya uchimbaji na hivyo leseni hiyo kumaliza muda wake tarehe 23/10/2018. Kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya mwaka 2010 na marekebisho yake ya mwaka 2017 eneo la leseni hiyo limerudishwa Serikalini baada ya kumaliza muda wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, mgodi katika eneo la Nyakafuru Wilayani Mbogwe utafunguliwa baada ya kampuni yaMabangu Mining Limited kuomba leseni ya uchimbaji wa madini kwa mujibu wa sheria na endapo Serikali itaridhia maombi hao, leseni itatolewa na shughuli inaweza kuanza, ahsante.