Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 44 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 365 2019-06-12

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-

Katika kujenga Tanzania ya viwanda, Serikali imekuwa na mikakati ya muda mrefu.

Je, ule mkakati wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI wa kujenga viwanda 100 kwa kila Mkoa ni sehemu ya mkakati na umeainishwa kwenye waraka gani wa Serikali ili kuwapa wananchi rejea ya pamoja ya kitaifa?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa kujenga viuwanda 100 kila MKoa ni sehemu ya mikakati mbalimbali inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano kujenga uchumi wa viwanda uliofungamanishwa na maendeleo ya watu. Ofisi ya Rais, TAMISEMI imeandaa mwongozo kubainisha majukumu Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa katika utekelezaji wa Sera ya viwanda. Lengo la mkakati huo ni kutoa hamasa kwa viongozi na wananchi kushiriki kikamilifu kuwezesha uwepo wa viwanda katika maeneo yao hivyo mkakati huo haupaswi kutenganishwa na mipango mingine ya Serikali inayohamasisha ujenzi wa viwanda nchini. Ahsante.