Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 43 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 363 2019-06-11

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:-

Eneo la Rubwera Kata ya Kyerwa ndiyo Makao Makuu ya Wilaya na maeneo mengi yalikuwa ya wananchi, kuna eneo lilichukuliwa na Jeshi la Magereza na wananchi walizuiliwa kufanya shughuli yoyote kwenye eneo hilo.

Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi hawa kama walivyoahidiwa?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Sebba Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa wakati wa uanzishwaji wa Wilaya mpya ya Kyerwa, eneo la wananchi wa Kijiji cha Rubwera Kitongoji cha Rwekorongo lilitolewa kwa ajili ya uanzishaji wa Gereza la Wilaya. Aidha, kwa mujibu wa tathmini ya Halmashauri ya Wilaya, jumla ya shilingi 661,928,640/= zinahitajika kuwafidia wananchi waliojitolea maeneo yao mwaka 2017.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni nia ya Serikali kuwalipa fidia wananchi wote nchini waliotoa maeneo yao kwa ajili ya kupisha ujenzi na au uanzishaji wa magereza ikiwemo wananchi wa Rubwera. Aidha, Serikali itaendelea kulipa fidia hizo kwa wananchi kwa awamu kutegemea na upatikanaji wa fedha kutoka kwenye bajeti ya Serikali.