Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 43 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 356 2019-06-11

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JORAM I. HONGOLI aliuliza:-

Mabaraza ya Usuluhishi ya Kata yamekuwa ni chanzo cha migogoro badala ya kutatua migogoro.

Je, ni nini mpango wa Serikali wa kutoa mafunzo ya muda mfupi ili waweze kumudu majukumu yao kwa ufanisi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joram Ismael Hongoli, Mbunge wa Lupembe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mabaraza ya Kata ni vyombo vya kisheria vya utatuzi wa migogoro katika ngazi ya chini ya jamii vyenye nguvu ya kisheria katika kutatua migogoro ya wananchi. Mabaraza hayo yaliyoanzishwa mwaka 1985 kwa Sheria ya Mabaraza ya Kata, Sura ya Namba 206 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, katika utekelezaji wa majukumu yake, baadhi ya Mabaraza yamekuwa na changamoto za kiutendaji zinazotokana na uelewa mdogo wa masuala ya kisheria kwa wajumbe, maadili na kutofahamu mipaka ya majukumu yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kukabiliana na changamoto hizo, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa mwaka wa fedha 2017/2018 ilitoa mafunzo kwa Wanasheria wa Halmashauri kuhusu usimamizi na uendeshaji wa Mabaraza ya Kata. Aidha, kwa mwaka wa fedha 2018/2019 Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa kushirikiana na Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo ilitoa mafunzo kwa Wakurugenzi na Wanasheria wa Halmashauri. Mpango wa Serikali ni kuendelea kutoa mafunzo kwa Mabaraza hayo kadri ya upatikanaji wa fedha, ahsante.