Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 41 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 338 2019-06-03

Name

Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA (K.n.y. MHE. MARTIN A. MSUHA) aliuliza:-

Uhaba wa walimu wa Hisabati na Sayansi umeathiri sana matokeo ya darasa la saba mwaka 2017 Wilayani Mbinga.

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka walimu wa masomo hayo Wilayani Mbinga?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA W. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Martin Alexander Msuha, Mbunge wa Mbinga Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, zipo sababu mbalimbali zilizopelekea kushuka kwa ufaulu wa wanafuzi wa darasa la saba wa mwaka 2017 Wilaya ya Mbinga ikiwemo. Upungufu wa walimu, ushiriki hafifu wa wazazi husasani kufatilia maendeleo ya watoto wao, utoro na nyingine nyingi. Walimu wa shule za msingi wanaoajiriwa wanaweza kufundisha masomo yote yaani Sanaa na Sayansi pamoja na Hisabati.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2017/2018 na 2018/2019 Serikali imeajiriwa walimu 14,422 ambapo 10,695 ni walimu wa shule za msingi za 3,727 ni walimu wa shule za sekondari. Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imepatiwa jumla ya walimu 143 kati hayo walimu 112 ni wa shule za msingi na walimu 31 ni wa shule za sekondari. Kati yao 28 ni wa Sayansi na Hisabati, mmoja masomo ya biashara na wawili ni walimu wa fasihi kiingereza (English Literature). Serikali itaendelea kuajiri walimu na kuwapanga kwenye Halmashauri hasa zenye upunugufu wa walimu kwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Ahsante.