Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 40 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 331 2019-05-31

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA (k.n.y. MHE. MASHIMBA M. NDAKI) aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa kila shule ya msingi au ya sekondari kunakuwa na walimu wa kike kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi wa kike hasa katika masuala yanayohusiana na hedhi salama?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mashimba Mashauri Ndaki, Mbunge wa Maswa Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inao utaratibu kupitia Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha kuwa katika kila shule ya msingi na sekondari wanateuliwa walimu wa kike wa kuwasaidia wanafunzi wa kike hususan katika masuala yanayohusiana na ushauri nasaha na unasihi likiwemo suala hilo. Lengo la kuwa na walimu hawa shuleni ni kuhakikisha kuwa wanafunzi wa kike wanapatiwa elimu ya afya na usafi itakayowawezesha kutambua mabadiliko yanayotokana na kupevuka kwa miili yao na kuelimishwa njia bora na salama za kujistiri pale wanapopatwa na hali hiyo. Aidha, wanafunzi hawa wanahitaji mlezi wa kike wa kuweza kuwasaidia wanapokuwa na changamoto mbalimbali kuhusiana na masuala ya kike.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia mpango wa Lipa Kulingana na Matokeo (Education Performance for Results - EP4R) imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya kusawazisha ikama ya walimu wakiwemo walimo wa kike katika Halmashauri ili kukabiliana na tatizo hilo.

Mheshimiwa Spika, ahsante.