Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 15 | Sitting 39 | Works, Transport and Communication | Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano | 327 | 2019-05-30 |
Name
Mattar Ali Salum
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Shaurimoyo
Primary Question
MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-
Kampuni ya Azam Marine ambayo inafanya biashara ya kusafirisha abiria kwa kutumia boti kupitia baharini, huuza tiketi kwa abiria kwa ajili ya safari lakini abiria anapochelewa safari tiketi hiyo huwa haitumiki na hivyo kusababisha hasara kwa abiria pamoja na usumbufu;-
(a) Je, Serikali inalijua hilo?
(b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo hilo?
Name
Eng. Atashasta Justus Nditiye
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muhambwe
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mattar, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali ina taarifa ya jambo hili kwa kuwa limekuwa likijitokeza mara kwa mara. Ufuatiliaji uliofanywa na Wizara yangu kupitia TASAC umebaini kuwa Kampuni iliyotajwa ina utaratibu wa namna abiria anavyoweza kuahirisha safari na namna nauli itakavyorejeshwa. Aidha, Kampuni hiyo imekuwa kuahirisha safari na namna nauli itakavyorejeshwa. Aidha, Kampuni imekuwa ikiruhusu abiria kutoa taarifa na kubadili muda wa safari bila gharama ya ziada ikiwa msafiri atatoa taarifa kabla ya chombo kuondoka. Utaratibu huu unatoa fursa kwa kampuni kuuza nafasi iliyoachwa wazi kwa wasafiri wengine ili kuepuka hasara.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa vyombo vya kampuni hii vimesajiliwa katika daftari la usajili linalosimamiwa na Mamlaka ya Bandari Zanzibar (ZMA), Wizara yangu kupitia TASAC itaendelea kufanya ufuatiliaji kwa kushirikiana na Wizara husika Zanzibar kupitia ZMA ili kusimamia utekelezaji wa utaratibu huu wa Kampuni ili uwasaidie abiria wanapoahirisha safari na kutoa taarifa kwa wakati.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved