Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 39 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 324 2019-05-30

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:-

Majengo ya Hospitali ya Wilaya ya Ulanga ni machache, madogo na machakavu hasa yale ya kulaza wagonjwa:-

Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ukarabati wa majengo hayo na ujenzi wa majengo mapya?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Goodluck Mlinga, Mbunge wa Ulanga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza kutekeleza mpango wa kuikarabati na kuipanua Hospitali ya Wilaya ya Ulanga ambapo mwezi Mei, 2019, Serikali imepeleka kiasi cha shilingi milioni 400 katika Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga kwa ajili ya ukarabati na upanuzi wa Hospitali ya Wilaya ya Ulanga. Aidha, katika mwaka wa fedha 2019/2020, Halmashauri imetenga shilingi milioni 60 kupitia mapato yake ya ndani kwa ajili ya kukarabati Hospitali ya Wilaya hiyo. Ahsante.