Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 37 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 313 2019-05-28

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:-

(a) Je, ni vijana wangapi kutoka Wilaya ya Kaskazini A na Wilaya ya Kaskazini B wamepata nafasi ya kujiunga na Jeshi kuanzia mwaka 2015?

(b) Je, mgawanyo wa idadi ya vijana wanaojiunga na Jeshi kwa kila wilaya nchini upoje?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka Mbunge wa Viti Maalum lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita yaani kuanzia mwaka 2015 hadi 2018 vijana walijiunga na JKT kutoka Zanzibar kwa kujitolea ni kama ifuatavyo:-

(i) Mwaka 2015/2016 vijana 300;
(ii) Mwaka 2016/2017 vijana 300;
(iii) Mwaka 2017/2018 vijana 400 kwa hivyo jumla katika miaka hiyo mitatu ni vijana 1000.

Jukumu la kugawa nafasi hizo kwa wilaya liko chini ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kwa mwaka 2019/20 Zanzibar imetengewa nafasi 500.

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, mgawanyo wa idadi ya vijana wanaojiunga na JKT kwa kujitolea kwa kila mkoa huzingatia uwiano wa idadi ya watu kulingana na takwimu za sensa ya Taifa ya watu na makazi, elimu, jinsia na sifa nyingine zinazokuwa zimeainishwa na mkuu wa JKT. Zoezi hili ikiwa ni pamoja na mgawanyo wa vijana hadi ngazi ya wilaya huratibiwa na wakuu wa mikoa husika baada ya Makao Makuu ya JKT kuainisha idadi ya vijana kwa kila mkoa.