Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 37 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 307 2019-05-28

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ufaulu wa wanafunzi katika maomo ya Sayansi na hisabati yanaonekana kushuka kila mwaka, mathalani mwaka 2015 asilimia 85 ya wanafunzi walifeli somo la hisabati matokeo ya kidato cha nne. Aidha, katika masomo mengine ya Kemia, Fizikia na Biolojia ufaulu bado ni duni sana.

(a) Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuinusuru Halmashauri ya Mji wa Tarime na janga hili la ufulu duni katika masomo ya sayasi?

(b) Je, nini mkakati wa Serikali katika kuiwezesha maabara za shule za sekondari zilizojengwa kwa nguvu kubwa ya wananchi ndani ya Jimbo la Tarime mjini kuweza kupata wataalam na vifaa vya maabara ili kuinuka ufaulu kwenye masomo ya Sayansi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko Mbunge wa Tarime Mjini lenye sehemu (a) na (b) kama ifutavyo:-

(a) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatekeleza mipango mbalimbali ya uboreshaji wa elimu ya sekondari nchini ili kuinua kiwango cha ufaulu na ubora wa elimu kwa ujumla. Serikali imeipatia Halmashuri ya Mji wa Tarime walimu 59 wa masomo ya sayansi ili kuboresha ufundishaji na ujifunzaji. Aidha, Serikali katika mwaka wa fedha 2019/20 imepanga kutumia shilingi bilioni 58.2 kupitia EP4R kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu ya elimu ya sekondari nchini ikiwemo Halmshauri ya mji wa Tarime. Vilevile kupitia mradi mpya wa uboreshaji wa Elimu ya Sekondari nchini, Serikali imepanga kutumia shilingi bilioni 48.9 kwa ajili ya kuboresha elimu ya sekondari nchini.

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, katika shule zote tisa za sekondari zilizopo katika Halmashauri ya Mji wa Tarime wanafunzi wanafanya mitihani ya masomo ya sayansi kwa vitendo kwa kutumia maabara zilizopo. Hata hivyo, maabara hizo ni kweli zinakabiliwa na upungufu wa vifaa vya maabara na huduma nyingine kama maji na gesi. Katika mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali kupitia mpango wa EP4R imepanga kutumia bilioni 58.2 kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu ya shule za sekondari ambapo jumla ya shule 70 zitapatiwa vifaa vya maabara zikiwemo shule za Halmashauri ya Mji wa Tarime.