Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 37 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 306 2019-05-28

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuza:-

Je, ni lini Serikali itaifanya Halmashauri ya Itigi kuwa Wilaya?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Massare Mbunge wa Manyoni Mangharibi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyoeleza wakati majibu swali la Bunge Na. 287 kuhusu pendekezo la kugawa Mkoa wa Tanga, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa Serikalli inatambua umuhimu wa kuanzisha maeneo mapya ya utawala kwa ajili ya kusogeza huduma karibu na wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, kwa sasa Serikali imeweka kipaumbele cha kuhakikisha maeneo yalianzisha hivi karibuni yanaboresha na kuendelezwa kwa miundombinu na huduma mbalimbali zikiwemo Ofisi, makazi ya viongozi na watendaji, huduma za afya, elimu, maji, mawasiliano, barabara na umeme ili wananchi waanze kunufaika na huduma zinazotolewa na Serikali kupitia mamlaka hizo.