Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 36 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 303 2019-05-27

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA III katika Kijiji cha Hemsambia na Vitongoji vyake vyote?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dunstan Luka Kitandula, Mbunge wa Mkinga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Vijiji vya Hemsambia na Kindundui ni miongoni mwa Vijiji vya Kata ya Kigongoi, Wilaya ya Mkinga vilivyofaidika na Awamu ya Tatu ya utekelezaji wa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini, REA III, mzunguko wa kwanza. Mkandarasi Kampuni ya Ubia ya JV Radi Service Limited, Njarita Contractor Limited na Aguila Contractor Limited yuko site anaendelea na kazi ya kusambaza umeme katika maeneo husika.

Mheshimiwa Spika, kazi za kupeleka umeme katika Vijiji vya hemsambia na Kindundui imejumuisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 2.1, njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa mbili, ufungaji wa transfoma mbili za KVA 50 pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 62. Gharama ya mradi ni shilingi milioni 184.23.

Mheshimiwa Spika, vijiji vingine vya Kata ya Kigongoi vya Vuga, Kwekuyu, Kindundui, Mgambo Shashui na Bombo Mbuyuni vitapatiwa umeme kupitia Mradi wa REA III Mzunguko wa Kwanza unaoendelea kutekelezwa Wilayani Mkinga na kukamilika mwezi Juni, 2020. Ahsante sana.