Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 36 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 302 2019-05-27

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE (K.n.y. MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA) aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA III katika Kata za Bujula, Nyamalimbe, Kamena, Nyalwanzaka, Nyakamwaga, Busanda Kaseme, Magenge, Butindwe na Nyaruyeye?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la mhesimiwa Lolesia Jeremiah Bukwimba, Mbunge wa Busanda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inapeleka umeme katika Jimbo la Busanda kupitia Mradi wa REA III Mzunguko wa Kwanza ambapo Kata ya Nyaruyeye itapatiwa umeme kupitia Mkandarasi Kampuni ya JV White City International Contractors. Na kazi ya kupeleka umeme katika Kata ya Nyaruyeye itakamilika mwishoni mwa Mwezi Mei, 2019 ambayo ni wiki hii.

Mheshimiwa Spika, katika Kata nyingine za Nyalwanzaja, Kamena, Busanda na Nyakamwaga zitapata umeme kupitia utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme katika vijiji vinavyopitiwa na mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa Gridi ya Taifa ya Msongo wa Kilovoti 220 kutoka Bulyanhulu hadi Geita. Hadi mwezi Mei, 2019 mkandarasi amekamilisha kazi za kufanya survey na kazi za ujenzi wa mradi zinatarajiwa kuanza mwezi Julai, 2019 na kukamilika mwezi Januari, 2021. Katika Kata zilizobaki za Magenge, Nyamalimbe, Bujula na Kaseme zitapatiwa umeme kupitia Mradi wa REA III Mzunguko wa Pili unaotarajiwa kuanza Mwezi Julai, 2019.