Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 36 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 301 2019-05-27

Name

Saul Henry Amon

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. DKT. TULIA ACKSON (K.n.y. MHE. SAUL H. AMON) aliuliza:-

Umeme wa REA umepita katika vijiji vya Unyamwanga, Kisonidzela na Mpuga lakini wananchi wa maeneo hayo hawajaunganishiwa huduma ya umeme.

Je, ni lini wananchi hao wataunganishiwa huduma ya umeme?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Saul Henry Amon Mbunge wa Rungwe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe ni miongoni mwa halmashauri zilizonufaika na utekelezaji wa mradi wa REA II uliotekelezwa na mkandarasi kampuni ya SINOTEC Ltd. kutoka nchini China ambapo vijiji vya Unyamwanga na Kisonidzela ni miongini mwa vijiji vilivyopatiwa huduma ya umeme.

Mheshimiwa Spika, kupitia utekelezaji wa mradi wa REA III mzunguko wa kwanza unaoendelea kutekelezwa na Mkandarasi STEG International Services jumla ya vijiji 26 katika Wilaya ya Rungwe vitafikishiwa umeme ikiwemo kijiji cha Mpuga.

Mheshimiwa Spika, kazi za mradi zinahusisha ujenzi wa kilomita 20 za njia ya umeme wa msongo kilovoti 33, kilomita 42 za njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4, ufungaji wa transfoma 25 na kuunganisha wateja wa awali 1,195. Gharama ya mradi ni shilingi bilioni 2.25

Mheshimiwa Spika, baadhi ya vitongoji ambavyo havikufikiwa na umeme katika utekelezaji wa REA II katika vijiji vya Unyamwanga na Kisonidzela vitapatiwa umeme kupitia mradi wa ujazilizi Awamu ya II Densification II utakaoanza na kutekelezwa kuanzia mwezi Julai, 2019 ahsante sana.