Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 36 Energy and Minerals Wizara ya Madini 300 2019-05-27

Name

Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:-

Wananchi wa Mtaa wa Mgusu wanaoishi ndani ya mipaka ya Mgodi wa Geita Gold Mine wanaathirika sana na uchafuzi wa mazingira unaotokana na taka zinazomwagwa katika maeneo karibu na wananchi.

Je, ni lini Serikali itatoa agizo kwa Geita Gold Mine kulipa wananchi fidia ili watoke katika eneo lililomilikishwa Mgodi?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini naomba nijibu swali la Mheshimiwa Upendo Furaha Peneza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa naomba nijibu kama swali lilivyoulizwa na kama ni marekebisho hayo anayoyasema Mheshimiwa Mbunge basi tunaomba arudishe swali alete jingine jipya tutamjibu kwa lile eneo lakini hapa tumemjibu kadri lilivyoulizwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mtaa wa Mgusu uko kilomita 4.5 kutoka eneo la uchimbaji la Nyamulilima Star and Comment la GGM ambapo kwa sasa uchimbaji unaendeshwa kwa niia ya chini kwa chini yaani Underground Mining Operations. Mawe ya Dhahabu yanayozalishwa katika eneo hilo hupelekwa kwenye eneo maalum la uchenjuaji yaani Processing plant ambalo lipo umbali wa kilomita 19 kutoka Mtaa wa Mgusu. Kwa umbali huo ni wazi kuwa ni vigumu kwa taka ngumu kufika katika Mtaa huo. Hata hivyo ukingo wa miamba isiyo na madini yaani Waste Rocks umewekwa ili kuzuia miamba hiyo kutoka nje ya eneo la uchimbaji.

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Madini ya Mwaka 2010, Kifungu cha 96(1) na 97(1)(a) na (b) vinaeleza kuwa, fidia inapaswa kulipwa kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi katika hatua ambapo muwekezaji anataka kuanza kuchimba madini baada ya kushauriana na Mamlaka ya Serikali za Mtaa husika na kujiridhisha juu ya madhara yanayoweza kusababishwa na uchimbaji huo.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Mtaa wa Mgusu wengi wao wanajishughulisha na uchimbaji mdogo wa madini. Hata hivyo tathimini ya mazingira iliyofanywa na mgodi wa GGM haionyeshi uwepo wa madhara yanayohitaji kuhamishwa kwa wananchi wa Kitongoji hicho. Aidha, Wizara kupitia Ofisi ya Madini Mkoa wa Geita itaendelea kusimamia na kukagua eneo hilo.