Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 34 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 286 2019-05-23

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:-

Wakati Jeshi la Polisi likitekeleza majukumu yake kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na hata uvunjifu wa Katiba kwa kisingizio cha maagizo kutoka juu:-

(a) Je, ni mamlaka gani iko juu ya sheria?

(b) Je, maagizo hayo yanapopingwa na sheria za nchi na kukiuka haki za binadamu nini hukumu ya yule aliyetendewa kinyume cha sheria?

(c) Je, huyu anayekutwa na kadhia hii hana haki ya kumjua huyo mwenye mamlaka ya juu?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka, Mbunge wa Liwale lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Spika, Jeshi la Polisi hutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo kwa msingi huo Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20 inampa mamlaka polisi kutumia nguvu ya wastani anapokuwa anatekeleza kazi yake kulingana na mazingira yaliyopo. Aidha, hakuna mamlaka ya juu katika Jeshi la Polisi iliyo juu ya sheria kiasi cha kuvunja sheria.

(b) Mheshimiwa Spika, nchi yetu inafuata misingi ya Demokrasia na Utawala Bora ambapo mtu yeyote anao uwezo wa kwenda kutoa malalamiko yake kwenye chombo chochote cha kisheria na hauta stahiki zikachukuliwa.

(c) Mheshimiwa Spika, hakuna mamlaka inayomzuia mtu kumuona mtu ambaye anadhani atamsaidia kutatua tatizo Lake Linalomsibu.