Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 34 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 281 2019-05-23

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU (K.n.y. MHE. SILYVESTRY F. KOKA) aliuliza:-

Shamba la uzalishaji wa Mitamba Kibaha lipo katikati ya Mji wa Kibaha na limezungukwa na makazi ya watu:-

Je, Serikali ina mpango gani juu ya matumizi ya eneo hili kwa ufanisi zaidi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais –TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Silvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali uliopo ni kutumia shamba la mitamba lililoko katika Halmashauri ya Mji wa Kibaha kwa ajili ya uzalishaji wa chanjo za mifugo na kuendelea kuimarisha kituo cha uhalishaji cha kanda ili kuendeleza Sekta ya Mifugo. Tayari Halmashauri imepima eneo la hekta 1,037 ambalo halijavamiwa na kupatiwa hati yenye namba 395140 ya mwaka 2011. Kwa sasa eneo hilo linatumika kwa majaribio na Tanzania Veterinary Laboratory Agency (TVLA) kwa ajili ya kufanya majaribio ya kuzalisha chanjo za magonjwa ya mifugo na kuweka kituo cha kanda cha uhamilishaji na tayari mitambo ya kuzalisha kimiminika cha hewa baridi ya nitrojeni imesimikwa. Ahsante.