Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 33 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 271 2019-05-22

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI (K.n.y. MHE. MENDRAD L. KIGOLA) aliuliza:-

Miundombinu ya shule nyingi za msingi katika Jimbo la Mufindi Kusini ni chakavu:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati miundombinu ya shule hizo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola, Mbunge wa Mufindi Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, moja ya changamoto kubwa zinazoikabili Sekta ya Elimu hapa Nchini ni uhaba na uchakavu wa miundombinu ya shule ikiwemo nyumba za walimu, vyumba vya madarasa pamoja na vyoo. Serikali kupitia Programu ya Lipa Kulingana na Matokeo katika Sekta ya Elimu (Education for Results – EP4R) inaweka kipaumbelea na kutenga bajeti kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu hiyo ya elimu.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2018/ 2019, Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imepokea jumla ya shilingi milioni 223.2 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu katika Shule za Msingi Kilolo na Makalala. Shule ya Msingi Kilolo ilipokea jumla ya shilingi milioni 136.6 kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu, ujenzi wa madarasa manne na ujenzi wa matundu sita ya vyoo na Shule ya Msingi Makalala imepokea jumla ya shilingi miloni 86.6 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa na matundu sita ya vyoo. Serikali itaendelea kutoa fedha kwa kadri ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya elimu ya msingi kulingana na upatikanaji wa fedha.