Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 32 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 268 2019-05-21

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanzisha Wilaya ya TANESCO katika halmashauri ya Mji wa Mafinga ili kukabiliana na kasi ya ukuaji (kiviwanda na kimakazi) wa Mji wa Mafinga?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA (K.n.y. WAZIRI WA NISHATI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi Mbunge wa Mafinga Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Mufindi ina halmashauri mbili ambazo ni Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi na Halmashauri ya Mji wa Mafinga. Katika halmashauri ya Mji wa Mafinga tayari ipo ofisi ya wilaya ya TANESCO inayotoa huduma kwa wananchi wa Mji wa Mafinga pamoja na wananchi wa Wilaya ya Mufindi. Kwa sasa, Ofisi ya TANESCO iliyopo Mafinga inakidhi mahitaji ya kutoa huduma kwa wananchi wote wa Mji wa Mafinga. Hata hivyo, Serikali kupitia TANESCO itaendelea kuboresha huduma za ofisi hiyo ili kukidhi ukuaji wa shughuli za biashara za wananchi wa Halmashauri ya Mafinga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kusogeza huduma zaidi kwa wananchi, TANESCO ilifungua ofisi ndogo (sub office) katika maeneo ya Igowole, Kibao na Mgololo. Ofisi hizi ni kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha huduma zinatolewa kwa urahisi kwa wananchi wa maeneo husika. Katika hatua za muda mfupi za kukabiliana na kasi ya ukuaji wa viwanda na makazi katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga, Serikali kupitia TANESCO imeongeza njia ya pili ya umeme (Ifunda Feeder) ya msongo wa kilovoti 33 kutoka kituo cha kupooza umeme cha Tagamenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hatua nyingine, TANESCO ina mpango wa kujenga kituo kikubwa cha kupooza umeme (Grid substation) katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga na Kazi ya upembuzi yakinifu imekamilika mwezi Januari, 2019 na ujenzi wa kituo unatarajiwa kukamilika Mwaka wa Fedha 2019/2020.