Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 32 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 265 2019-05-21

Name

Machano Othman Said

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. MACHANO OTHMAN SAID aliuliza:-

Kwa muda mrefu kumekuwa na upungufu mkubwa wa Wafanyakazi wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar hali inayopunguza ufanisi wa kazi katika Idara hiyo?

(a) Je, ni lini Serikali itaajiri Wafanyakazi wa kutosha katika Idara hiyo?

(b) Je, ni lini Serikali itaimarisha Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Mjini Magharibi ili kupunguza msongamano katika Ofisi kuu ya Uhamiaji Zanzibar?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Machano Othman Said Mbunge wa Baraza la Wawakilishi lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Idara ya Uhamiaji imetengewa Bajeti ya kuajiri Watumishi 505 katika mwaka wa fedha 2018/2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika mwaka wa fedha 2017/2018 Idara ya Uhamiaji limefanya upanuzi wa Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Mjini Magharibi kwa kuongeza vyumba vitatu kwa ajili ya kuimarisha huduma za Kiuhamiaji ikiwemo huduma ya pasipoti mtandao, pia katika Bajeti ya mwaka huo Idara ya Uhamiaji imetenga fedha kwa ajili ya upanuzi wa Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Mjini Magharibi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hatua hiyo Idara itakuwa imeongeza wafanyakazi, pia Ofisi ya Uhamiaji Mjini Magharibi itaimarika ili kupunguza msongamano uliopo katika Ofisi kuu ya Uhamiaji Zanzibar.