Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 31 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 261 2019-05-20

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:-

Je, Megawati moja ya umeme inazalishwa kwa bei gani na inauzwa kwa bei gani (unit cost)?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA (K.n.y. WAZIRI WA NISHATI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Lwehikila Theonest, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Shirika la Umeme Nchini, inagharamia uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme hadi kwa mteja kwa kuweka miundombinu husika ya umeme. Kwa sasa gharama ya kuzalisha uniti moja (Kwh) ya umeme kwa kutumia chanzo cha maji ni shilingi 36 na gharama ya kuzalisha uniti moja ya umeme kwa kutumia gesi asilia ni wastani wa shilingi 150. Gharama ya kuzalisha uniti moja kwa mitambo inayotumia mafuta ya dizeli katika maeneo yaliyopo nje ya Gridi ya Taifa ni shilingi 720 kwa uniti moja yaani Kwh moja.

Mheshimiwa Spika, bei ya kuuza umeme inatokana pia na gharama za kuzalisha, kusafirisha na kusambaza umeme. Kwa sasa bei ya kuuza umeme ni wastani wa shilingi 242 kwa uniti yaani Kwh.