Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 31 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 254 2019-05-20

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI aliuliza:-

Tangu Wilaya ya Kilolo ipate hadhi ya kuwa wilaya mwaka 2002 Serikali haijaweza kujenga ofisi za polisi na nyumba za kuishi yalipo Makao Makuu ya Wilaya:-

Je, ni lini Serikali itajenga ofisi na nyumba hizo za polisi Wilaya ya Kilolo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ritta Kabatti, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Polisi lina jumla ya wilaya 168 za kipolisi na zile za Kiserikali, kati ya hizo 127 zina majengo kwa ajili Ofisi na vituo vya polisi na wilaya 41 zilizobaki hazina majengo kwa ajili ya ofisi na vituo vya polisi wilaya ikiwemo Wilaya ya Kilolo. Hii in atokana na ufinyu wa bajeti ya maendeleo kwa Jeshi la Polisi.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Jeshi la Polisi limejikita kukamilisha miradi iliyokwisha anzishwa huko nyuma, pindi miradi hiyo itakapokuwa imekamilika na hali ya kibajeti itakapokuwa imeimarika Jeshi la Polisi litajikita katika ujenzi wa vituo vya polisi vya wilaya pamoja na nyumba za askari katika wilaya ambzo hazina majengo hayo ikiwemo Wilaya ya Kilolo.