Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 9 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 116 2019-09-13

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA (K.n.y. MHE. DEVOTHA M. MINJA) aliuliza:-

Timu ya Taifa ya Wanawake Twiga Stars imefanya vizuri na kuliletea Taifa heshima miaka iliyopita hivi karibuni:-

Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuhamasisha soka kwa wanawake katika ngazi za wilaya na mikoa kuwa na timu za soka za wanawake kama ilivyo kwa wanaume?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Devotha Mathew Minja, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Timu ya Soka ya Taifa ya Mwanawake (Twiga Stras) pamoja na ile ya Kilimanjaro Queens miaka ya hivi karibuni zimefanya vizuri na kuliletea taifa heshima. Kwa kutambua mchango wa wanawake katika kukuza soka la nchi yetu Serikali kwa kushirikiana na wadau hususani Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini Tanzania, imejipanga kutekeleza yafuatayo:-

(i) Serikali inaendelea kusajili vyama na vilabu mbalimbali vya michezo pamoja na kutoa wito kwa wananchi kuendelea kusajili vilabu vyao vikiwemo vya soka la wanawake;

(ii) Serikali imeendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wananchi wote kushiriki katika michezo ukiwemo mpira wa miguu kwa wanawake;

(iii) Serikali kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT) limeendelea kujenga mazingira mazuri kwa vyama na mashirikisho ya michezo kufaya kazi zao. Baraza la Michezo la Taifa (BMT) pia wameridhia kuanzishwa kwa ligi ya wanawake ya mpira wa miguu;

(iv) Mafunzo mbalimbali ya ukocha na uamuzi wa mpira wa miguu kwa wanawake yametolewa na kwamba tunao wanawake waamuzi (referees) wanaotambulika na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA).

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuwahamasisha wanawake kujihusisha katika kucheza mpira wa miguu kwa kuwa ni mchezo maarufu na kwamba utatoa fursa ya ajira kwa mtoto wa kike.