Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 108 2019-09-13

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:-

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuna upungufu mkubwa wa watumishi wa sekta ya afya:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo hilo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lolesia Jeremiah Bukwimba, Mbunge wa Busanda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017 hadi 2018/2019, Serikali imeajiri watumishi 8,444 wa sekta ya afya nchini ambapo watumishi 45 walipangwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita. Katika mwaka wa fedha 2019/2020, Ofisi ya Rais, TAMISEMI imepata kibali cha kuajiri watumishi 550 wa sekta ya afya na taratibu zinakamilishwa ili waweze kupangwa kwenye vituo vya kutolea huduma kote nchini ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuajiri watumishi wa kada mbalimbali za afya kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.