Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 7 Water and Irrigation Wizara ya Maji 97 2019-09-11

Name

Christopher Kajoro Chizza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ENG. CHRISTOPHER K. CHIZA Aliuliza:-

Serikali ilitoa zaidi ya shilingi bilioni mbili kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maji ya Nyabibuye, Gwanumpu, Muhange, Kiduduye, Nyangwijima na Kakonko Mjini. Miradi hiyo sasa inahitaji ukarabati mkubwa hata kabla ya kuanza uzalishaji na mingine utekelezaji upo chini ya asilimia 10:-

(a) Je, ni kasoro gani zimesababisha miradi yote sita kutotekelezwa kwa mwaka uliopangwa?

(b) Serikali imechukua hatua gani kuhakikisha miradi hiyo inakamilika?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Christopher Chiza Mbunge wa Buyungu, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa miradi ya Muhange, Kiduduye na Nyangwijima ulikamilika lakini ulishindwa kuwanufaisha wananchi kutokana na kasoro mbalimbali zilizojitokeza ikiwemo eneo la kisima cha pampu cha mradi wa Muhange kujaa tope; na pia kwa mradi wa maji Nyagwijima na Kiduduye eneo la chanzo kushindwa kuzuia maji kuyapeleka kwenye kisima chenye pampu hii imetokana na matatizo ya usanifu yaliyojitokeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha miradi hii inatoa huduma kwa wananchi kama ilivyokusudiwa, Serikali imechukua hatua mbalimbali kwa miradi ya Muhange, Kiduduye na Nyagwijima, Wizara imefanya mapitio ya usanifu ambapo kiasi cha shilingi milioni 300 kimekadiriwa ili kurekebisha kasoro zilizojitokeza. Tayari Serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni 120 kwa ajili ya maboresho ya mradi wa maji Muhange ambapo utekelezaji unaendelea na umefikia asilimia 45. Serikali itaendelea kutenga na kutoa fedha kwa ajili ya kuboresha pia miradi ya Nyagwijima na Kiduduye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi ya maji Gwanumpu, Nyabibuye na Kakonko Mjini utekelezaji wake ulichelewa kutokana na wakandarasi kujenga miradi hiyo kwa kasi ndogo kutokana na uwezo mdogo wa kifedha. Hali hii ilisababisha baadhi kusitishwa mikataba yao. Mkandarasi wa Mradi wa Gwanumpu yupo eneo la mradi na anaendelea na kazi ambapo amefikia asilimia 40. Kwa Mradi wa Maji wa Nyabibuye na Kakonko Mjini taratibu za kusaini mikataba na wakandarasi wapya zinaendelea ili waweze kukamilisha utekelezaji wa miradi hiyo.