Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 94 2019-09-11

Name

Azza Hilal Hamad

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA (K.n.y. MHE. AZZA H. HAMAD) aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itawapa huduma ya umeme wananchi wa Vijiji vya Buyubi, Itwangi, Imenya, Nyambui na Mwankanga ambao muda mrefu wamekuwa watazamaji wa nguzo za umeme unaokwenda maeneo mengine?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Azza Hillal Hamad, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa kufikisha umeme katika vijiji vyote nchini vikiwemo vijiji 126 vya Wilaya ya Shinyanga Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji 22 kati ya vijiji 126 katika Wilaya ya Shinyanga Vijijini vina umeme. Vijiji 50 vitapatiwa umeme kupitia Mradi wa REA III, Mzunguko wa Kwanza unaotekelezwa na Mkandarasi Angelique International Limited ambapo hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Agosti, 2019 jumla ya vijiji 19 vimeshawashiwa umeme na ujenzi wa miundombinu unaendelea katika vijiji vilivyobaki na wateja zaidi ya 211 wameunganishiwa umeme. Kazi ya kupeleka umeme katika vijiji hivi itakamilika ifikapo mwezi Juni, 2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya kupeleka umeme katika vijiji 50 vya Wilaya ya Shinyanga Vijijini inahusisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 170.9; ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 156; ufungaji wa transfoma 78 za KVA 50 na KVA 100 na kuunganisha umeme wateja wa awali 2,241. Gharama za mradi ni shilingi bilioni
10.7 na mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji 54 vilivyobaki vikiwemo vijiji vya Buyubi, Itwangi, Imenya, Nyambui na Mwankanga vitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA III, Mzunguko wa Pili unaotarajia kuanza mwezi Januari, 2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.