Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 27 2016-01-27

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. LOLESIA J. M. BUKWIMBA aliuliza:-
Je, ni lini miradi ya usambazaji wa umeme katika Kata za Kamena, Nyamalimbe, Busanda, Nyakamwaga, Nyakagomba, Nyaruyeye, Kaseme, Magenge, Nyalwanzaja na Bujula katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita utaanza rasmi?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa napenda kujibu swali la Mheshimiwa Lolesia Jeremiah Maselle Bukwimba, Mbunge wa Jimbo la Busanda, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Kanda za Busanda na Nyakamwaga zinafanyiwa tathmini ya Kampuni ya Ramaya International Tanzania Limited na zimewekwa kwenye Mpango wa Mradi wa Geita – Nyakanazi Transmission Line.
Mheshimiwa Spika, kazi ya kupeleka umeme kwenye Kata za Busanda na Nyakamwaga, itajulimsha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 23.7; pamoja na ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 wenye urefu wa kilomita 18.5; lakini kadhalika, ufungaji wa transfoma sita ambapo transfoma moja ina ukubwa wa kVA 50; transfoma mbili mbazo zina ukubwa wa kVA 100 na transfoma tatu zenye ukubwa wa kVA 200.
Mheshimiwa Spika, gharama ya kazi hii inakadiriwa kuwa shilingi bilioni 1.6. Kazi inatarajia kuanza mwezi Oktaba mwaka huu wa 2016 na itakamilika mwaka 2018.
Mheshimiwa Spika, Kata za Kamena, Nyamalimbe, Kaseme pamoja na Nyarwanzaga, zimefanyiwa tathmini na kubainika kuwa kazi ya kupeleka umeme kwenye Kata hizo itajumuisha ujenzi wa njia ya umeme msongo kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 50.8. Kadhalika ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 25, pamoja na ufungaji wa transfoma 11 ambapo transfoma tatu zaina ukubwa wa kVA50; transfoma sita zina ukubwa wa kVA 100 na tranfoma mbili zenye ukubwa wa kVA200. gharama ya kazi hii ni shilingi bilioni 2.87.
Mheshimiwa Spika, Kata hizi zimo pia katika mpango wa awamu ya tatu ya kusambaza umeme vijijini yaani REA - Phase III unaotajariwa kukamilika mwezi Julai, 2016.
Mheshimiwa Spika, tathmini ya mahitaji halisi kwa ajili ya kupeleka umeme katika Kata za Nyaruyeye, Magenge, Nyakagomba na Bujula inafanywa na TANESCO na itakamilika mwezi Machi, mwaka huu ili kujumlishwa katika Mradi wa Awamu ya Tatu wa Kusambaza Umeme Vijijini yaani REA-Phase III unaotarajiwa pia kuanza mwezi Julai, mwaka 2016.