Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 83 2019-09-10

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE Aliuliza:-

Mradi wa REA III(1) unatekelezwa katika Jimbo la Tabora Kaskazini kwa kasi ndogo na mpaka sasa ni vijiji vitatu tu kati ya vijiji 82 ndiyo vimewashwa umeme.

(a) Je, Serikali inachukua hatua gani kumfanya mkandarasi akamilishe kuwasha umeme katika vijiji vyote 18 vya REA III(1)?

(b) Kwa vile kwa makosa Mradi wa REA III(1) unarudiwa kupelekwa katika Kijiji cha Upuge, Kata ya Upuge ambako umeme ulishapelekwa na REA III. Je, ni lini sasa umeme utapelekwa katika Kata ya Ikongolo ambako ni Kata jirani na Kata ya Upuge?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI Alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Almasi Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa kufikisha umeme katika vijiji vyote nchini vikiwemo vijiji vya Jimbo la Tabora Kaskazini. Katika Jimbo la Tabora Kaskazini, Vijiji 18 vitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA III(1) unaoendelea kutekelezwa na Mkandarasi Kampuni ya JV Pomy Engineering Company Limited, Intercity Builders Limited na Octopus Engineering Limited. Ili kuhakikisha mkandarasi anakamilisha kazi za kuwasha umeme katika vijiji 18 vinavyofanyiwa kazi, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na TANESCO wameimarisha usimamizi wa kazi za kila siku za mkandarasi na kumtaka mkandarasi kuwa na vifaa kwa ajili ye ujenzi wa mradi kutoka ndani ya nchi.

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Vijiji vya Kata ya Ikongolo vinavyojumuisha Kanyenye, Kiwembe na Majengo vitapelekewa umeme kupitia utekelezaji wa Mradi wa REA III(2) utakaoanza mwezi Januari, 2020. Kazi ya kupeleka umeme katika vijiji vya kata hizo utahusisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovolt 33 yenye urefu wa kilometa 36.14, njia ya umeme wa msongo wa kilovolti 0.4 yenye urefu wa kilometa 20.28, ufunguaji wa transfoma tisa za KVA 50 na KVA 100 pamoja na kuwanungnishia umeme wateja wa awali 614 na gharama ya mradi huu ni shilingi bilioni 2.29.