Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 65 2019-09-09

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:-

Ujenzi wa Bwawa la Matwiga Wilayani Chunya umechukua zaidi ya miaka mitano bila kukamilika:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi huo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Victor Mwambwalaswa, Mbunge wa Jimbo la Lupa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Chunya ni miongoni mwa wilaya zenye asilimia ndogo ya upatikanaji wa huduma ya maji vijijini. Changomoto hii inatokana na wilaya hiyo kuwa na uhaba mkubwa wa vyanzo vya maji ikiwemo mito na chemchem ambazo zingeweza kutumiwa kuhudumia wananchi. Aidha, wilaya hii pia inakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa maji chini ya ardhi. Kwa kutambua hilo, Serikali ilianza ujenzi wa mradi wa maji wa Bwawa la Matwiga kwa lengo la kusaidia kupunguza shida ya maji iliyopo. Utekelezaji wa mradi huo ulipangwa katika awamu mbili ambapo awamu ya kwanza ilijikita katika ujenzi wa bwawa lenyewe kama chanzo cha maji na awamu ya pili ni ujenzi wa miundombinu ya kusambaza maji kutoka kwenye bwawa kwenda kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa awamu ya kwanza inayohusisha ujenzi wa bwawa lenyewe imekamilika ambapo bwawa hilo lina uwezo wa kuhifadhi maji lita 248,000,000 kwa mwaka. Hata hivyo, mnamo mwaka 2018 kulikuwepo na changamoto ya mvua kubwa iliyopekelea kuharibika kwa sehemu ya utoro wa maji (Spillway) ambayo kwa sasa mkandarasi (DDCA) yupo eneo la kazi na anaendelea na marekebisho ambapo kabla ya msimu wa mvua za mwaka huu kazi hiyo itakuwa imekamilika.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza utekelezaji wa awamu ya pili inayohusu ujenzi wa miundombinu ya kupeleka maji kwa wananchi. Ili kutumiza azma hiyo, Serikali imengia mkataba na Mtaalam Mshauri, BICO kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kufanya usanifu wa miundombinu ya kusambaza maji. Hadi sasa Mtaalam Mshauri huyo amewasilisha taarifa ya awali ya usanifu wa miundombinu ya kusambaza maji katika vijiji vinne (4) vya Kata za Matwiga na Mtanila. Kukamilika kwa hatua ya usanifu kutawezesha Serikali kutenga na kupeleka fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa miundombinu ya kusambaza maji.