Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 79 2019-11-12

Name

Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA aliuliza:-

Mradi wa Maji unaotekelezwa chini ya Programu ya WSDP katika Vijiji vya Malinyi, Kipingo na Makerere unasuasua sana toka 2015 hadi sasa mradi huo haujakamilika:-

(a) Je, ni lini mradi huo utakamilishwa ili kuwawezesha wakazi wapatao 18,000 wa vijiji hivyo kupata maji safi na salama?

(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapelekea maji wakazi wa Vijiji vya Miembeni, Mchangani na Misegese Kata ya Malinyi?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Hadji Hussein Mponda, Mbunge wa Jimbo la Malinyi, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuanzia mwaka 2015, Serikali inatekeleza mradi wa maji wa Malinyi unaotarajia kuhudumia Vijiji vya Kipingo, Makerere na Malinyi ambapo ni Makao Makuu ya Wilaya. Ujenzi wa mradi huo unagharimu shilingi bilioni 3.01. Hadi kufikia mwezi Oktoba, 2019, utekelezaji wake umefikia asilimia 80. Kazi zilizofanyika ni ujenzi wa miundombinu ya chanzo cha maji, ulazaji wa bomba kuu la maji urefu wa kilomita 22, ujenzi wa tanki la lita 150,000, vituo vya kuchotea maji 47 na ulazaji wa mabomba ya usambazaji maji kwa umbali wa kilomita 14.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kukamilika kwa kazi hizo, miundombinu hiyo imeshindwa kufikisha huduma ya maji kwa wananchi kutokana na upungufu katika usanifu wa mradi. Serikali imemwagiza Mtaalam Mshauri anayesimamia ujenzi wa mradi huo kufanya marekebisho ili wananchi waweze kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Vijiji vya Mwembeni, Misegese na Mchangani kuna visima virefu viwili vyenye maji ya kutosha. Hivyo, kwa mwaka huu wa fedha 2019/2020 Serikali itafanya usanifu ili kuviendeleza visima hivyo ili kuboresha huduma ya maji kwa wananchi wa vijiji hivyo. (Makofi)