Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 73 2019-11-12

Name

Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARY D. MURO aliuliza:-

Viwanja vya Mwanalugali Mjini Kibaha vimeshindwa kupimwa kutokana na mgogoro uliopo kwa wenye ardhi hiyo kutolipwa fidia wakati wa upimaji mwaka 2000:-

Je, Serikali inatoa msaada gani kwa wananchi hao ambao wameshindwa kuendeleza maeneo yao na kuwasababishia umaskini mkubwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mary Deo Muro, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha uthamini na kubaini watu 62 wanadai fidia kiasi cha Sh.575,017,858. Serikali imepanga kulipa fidia hiyo kwa kutumia fedha zitatokana na mauzo ya viwanja vilitolewa kwa wananchi na taasisi tangu mwaka 2004 lakini mpaka leo bado havijalipiwa na havilipiwi kodi ya Serikali.

Aidha, Serikali inakusudia kubadili matumizi ya eneo moja la ibada ambalo wananchi wanadai fidia ili wananchi wamilikishwe maeneo yao. Vilevile, Halmashauri inakusudia kuomba kibali kwa Kamishna wa Ardhi ili kufuta baadhi ya viwanja ili viweze kuuzwa kutunisha Mfuko wa Fidia na vingine kukabidhiwa kwa wananchi wanaodai fidia ili kumaliza mgogoro uliokuwepo kwa muda mrefu.