Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 5 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 70 2019-11-11

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:-

Serikali imeruhusu urasimishaji wa makazi katika maeneo mbalimbali Nchini ikiwemo Jiji la Mwanza isipokuwa maeneo ya Kata ya Isamilo, Mbugani, Mabatini na Igogo.

Je, ni lini Serikali itawamilikisha wananchi hawa maeneo yao kwa kuwa wameishi katika maeneo haya kwa muda mrefu?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendele ya Makazi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula, Mbunge wa Nyamagana kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na zoezi la urasimishaji wa makaziyasiyopangwa katika maeneo mbalimbali nchini ikiwa ni utekelezaji wa kifungu namba6.4.1(iii) cha Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995 ambacho kinatamka kwamba;

“Maeneo ya makazi holela isipokuwa yale yaliyojengwa kwenye maeneo ya hatarishi hayatabomolewa bali yataboreshwa na kuwekewa huduma za msingi”.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Jiji la Mwanza urasimishaji wa makazi unafanyika katika kata mbalimbali zikiwemo Kata za Isamilo na Mbugani. Katika Kata ya Isamilo urasimishaji umefanyika katika Mitaa ya Msikiti, SDA pamoja na National ambapo michoro ya mipangomiji miwili yenye jumla ya viwanja 3,444 imeandaliwa, viwanja 560 vimepimwa na viwanja 101 tayari vimemilikishwa. Aidha, Katika Kata ya Mbugani urasimishaji umefanyika katika Mitaa ya Nyashana na Kasulu ambapo michoro miwili ya mipangomiji yenye jumla ya viwanja 1001 iliandaliwa na viwanja 395 vimepimwa na vipo katika hatua ya umilikishaji.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kufanyika urasimishaji katika mitaa hiyo, maeneo mengine ya kata za Isamilo, Mbugani, Igogo na Mabatini hayajafanyiwa urasimishaji wa makazi kutokana na sehemu kubwa ya maeneo hayo kuwa hatarishi; ambayo yapo kwenye milima yenye miteremko mikali zaidi ya asilimia 15. Hivyo maeneo hayo hayakidhi vigezo vya kurasimishwa kwa kuwa ni hatarishi kwa maisha ya wananchi na mali zao pamoja na ugumu wa kuyafikika kwa barabara.

Mheshimiwa Spika, Mpango Kabambe wa Jiji la Mwanza 2015/2035 umeainishabaadhi ya maeneo ya Kata za Mbugani, Isamilo, Pamba, Nyamagana, Mkuyuni na Igogo kuwa ni maeneo yanayotakiwa kuendelezwa upya (redevelopment) kwa kuzingatia hali halisi ya miinuko na ujenzi hatarishi uliofanyika. Kwa sasa wamiliki wamakazi hayo watatambuliwa na kupatiwa leseni za makazi (formalization)wakati wakisubiri uendelezwaji mpya wa maeneo hayo.