Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 47 2019-11-08

Name

Saed Ahmed Kubenea

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Ubungo

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST (K.n.y. MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:-

Gesi asilia iliyogundulika nchini ni takribani ujazo wa trilioni feet 56:-

(a) Je, uwekezaji wa viwanda vinavyotumia gesi asilia kwa ukanda wa Kusini umefikia wapi na ni wa kiwango gani?

(b) Je, mpango wa kujenga kiwanda cha kuchakata gesi asilia bado upo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Saed Ahmed Kubenea, Mbunge wa Jimbo la Ubungo, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, gesi asilia iliyogundulika nchini hadi sasa ni futi za ujazo trilioni 57.54. Mikoa ya Lindi, Mtwara, Pwani na Dar es Salaam ni maeneo yaliyonufaika na shughuli za uwekezaji katika viwanda vinavyotumia gesi asilia. Matumizi ya gesi asilia nchini yalianza tangu mwaka 2004 ambapo kufikia mwezi Oktoba, 2019, jumla ya viwanda 48 vimeunganishwa na mtandao wa gesi asilia. Viwanda hivyo vinatumia gesi asilia kama nishati na vingine vinazalisha umeme kwa matumizi ya viwanda.

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa mradi wa kusindika gesi asilia kuwa kimiminika (LNG) unaendelea. Kwa sasa utekelezaji wake umefikia hatua ya majadiliano ya mkataba wa nchi husika (Host Government Agreement) kati ya wawekezaji na Serikali. Ahsante.