Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 43 2019-11-08

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE (MHE. AMINA S. MOLLEL) aliuliza:-

Shule ya Viziwi Mwanga hutoa Elimu ya Msingi kwa Watoto wasiosikia na wasioongea kwa Mikoa ya Kilimanjaro, Tanga na Arusha; wanapohitimu Elimu ya Msingi, Wanafunzi hao hujiunga na Shule za Sekondari za kawaida ambazo hazina Walimu wenye Taaluma Maalum, vifaa na mazingira rafiki kwa Watoto wenye ulemavu:-

Je, ni lini Serikali itajenga Shule ya Sekondari Maalum kwa Watoto Viziwi (wasiosikia na wasioongea)?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Prof. Jumanne Abdallah Maghembe Mbunge wa Mwanga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu kwa wanafunzi viziwi inatolewa katika Shule maalum 17 za Msingi na vitengo maalum 120. Shule hizi za Msingi zina jumla ya wanafunzi 7,212 na jumla ya walimu 885 wataalam wa kufundisha wanafunzi viziwi. Vilevile, ipo Shule maalum moja ya Sekondari na vitengo maalum 23 vya sekondari. Shule hizi za sekondari zina jumla ya wanafunzi viziwi 1,778 na jumla ya walimu 302 wataalam wa kufundisha wanafunzi viziwi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha ujenzi wa Shule ya Sekondari Maalum ya Viziwi iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Meru katika eneo la Tengeru (Patandi), ambayo mwaka 2020 kwa mara ya kwanza itaanza kudahili wanafunzi viziwi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kutoa wito kwa wadau wote wa elimu wenye nia ya kujenga Shule za Watoto wenye ulemavu wakiwemo viziwi, wafanye hivyo, Serikali itatoa vibali husika kwa kuzingatia taratibu na sheria husika.