Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 42 2019-11-08

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya King’ori kutoka Malula Kibaoni hadi King’ori Madukani, Maruvango, Leguruki, Ngaranyuki hadi Uwiro?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Wilaya ya Meru imekamilisha usanifu wa barabara ya Malula-King’ori-Leguki-Ngarenanyuki yenye urefu wa Kilomita 33 ili kuijenga kwa kiwango cha changarawe kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.259 ili ipitike majira yote ya mwaka. Serikali inaendelea kutafuta fedha za kukamilisha ujenzi huo. Aidha, ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami ni mpango wa muda mrefu ambao utekelezaji wake utategemea upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikitoa fedha kwa ajili ya matengenezo ya kawaida ya barabara hiyo katika mwaka wa fedha 2017/2018 kiasi cha shilingi milioni 221 kilitumika kufanya matengenezo ya kawaida katika barabara hiyo. Vilevile mwaka wa fedha 2019/2020 kiasi cha Shilingi milioni 35.7 kimetengwa kwa ajili ya matengenezo ya kawaida.