Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 40 2019-11-08

Name

Justin Joseph Monko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. JUSTIN J. MONKO aliuliza:-

Inapotokea Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa/Kijiji amefariki au kupoteza sifa ya kuwa Mwenyekiti wa Mtaa au Kijiji husika huongozwa na Kaimu Mwenyekiti:-

Je, kwa nini Serikali haioni umuhimu wa kuwepo uchaguzi mdogo kama ilivyo kwa Madiwani na Wabunge?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MIAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Justin Joseph Monko, Mbunge wa Singida Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa za Mwaka 2019 yaani Kanuni ya 43(1) – (4) na Kanuni ya 45 zinatoa fursa ya kufanya Uchaguzi Mdogo kujaza nafasi iliyoachwa wazi endapo Mwenyekiti wa Kitongoji, Kijiji, Mtaa atafariki au kupoteza sifa za kuendelea kuwa katika nafasi hiyo kutokana na sababu zilizoainishwa kwenye Kanuni ya 44(1) na (2). Uchaguzi Mdogo hautafanyika endapo muda uliosalia kabla ya muda wa Mwenyekiti kuwa kwenye madaraka kukoma ili kupisha uchaguzi ni miezi sita au pungufu yake. Ahsante.