Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 3 Radio and Television Broadcasting Services Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 38 2019-11-07

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:-

TBC ni Shirika la Umma na hutangaza habari na vipindi mbalimbali ili Watanzania wasikie kwa Lugha ya Kiswahili; Tanzania pia ina wageni kutoka nchi mbalimbali duniani waishio nchini. Lakini TBC limekuwa likitangaza taarifa za habari na vipindi vyake vingine kwa lugha ya Kiswahili tu; zamani kulikuwa na kipindi cha External Service kilichokuwa kikitangazwa kwa Lugha ya Kiingereza ili wageni waishio nchini wasikie lakini sasa hivi hakipo.

(a) Je, ni kwa nini TBC ilifuta kipindi cha External Service kilichokuwa kikitangaza taarifa ya habari kwa Lugha ya Kiingereza?

(b) Je, kwa kutangaza taarifa ya habari kwa Kiswahili tu hatuoni kwamba tunawanyima wageni fursa ya kujua kinachoendelea nchini?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwani niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo napenda kujibu swali la Taska Restituta Mbogo Mbunge wa Viti Maalum lenye vipengele (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Idhaa ya External Service ya Radio Tanzania Dar Es Salaam ilianzishwa rasmi wakati wa harakati za kupigania uhuru katika nchi za kusini mwa Afrika ikiwepo, Msumbiji, Zimbabwe, Namibia, Angola, Afrika ya Kusini. Viongozi wa wapigania uhuru katika nchi hizo waliishi na kuratibu harakati za ukombozi kutokea Tanzania ambapo walirusha ya Radio ya kuhamasisha wananchi wao kushiriki katika mapambano hayo kupitia Idhaa hiyo ya External Service. Baada ya nchi hizo kupata uhuru, Idhaa hiyo haikuendelea tena na hayo matangazo yake.

(b) Hata hivyo, kwa sasa TBC kupitia stesheni yake ya TBC International inayopatikana katika masafa ya 95.3, hutangaza kwa lugha ya Kiingereza. Aidha, TBC1 pamoja na TBC Taifa zinarusha baadhi ya vipindi kwa Kiingereza. Kwa mfano TBC1 ina vipindi maarufu “This Week in Perspective” na “International Sphere” na TBC Taifa ina vipindi ya”Breakfast Express”, “Daily Edition”, “Day Time” Overdrive kwa Kiingereza. Vipindi hivi huzungumzia masuala mbalimbali yakiwepo ya kisiasa, kiuchumi, pamoja na kijamii.

(c) Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kwa kutangaza taarifa ya habari kwa lugha moja ya Kiswahili kunawanyima wageni fursa ya kujua masuala mbalimbali yanayoendelea hapa nchini. Lakini yapo magazeti mbalimbali yanayochapisha habari hizo zinazotokea nchini kwa lugha ya Kiingereza. Magazeti hayo ni pamoja na Daily News, The Guardian, The Citizen.